DR Congo


Watu wengine 50 wamenusurika
Watu 50 wamefariki nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo baada ya boti kuzama kwenye mto kaskazini mwa nchi hiyo.
Kwa mujibu wa Richard Mboyo Iluka, naibu gavana wa jimbo la Tshuapa, boti hilo lilikuwa limewabeba abiria wengi, wengi wao wafanyabiashara, waliokuwa wanasafiri kutoka eneo la Monkoto kwenda Mbandaka.
Amesema watu wengine 50 wamenusurika.
Gavana huyu amesema hadi sasa hawajafahamu chanzo cha ajali hiyo.
Kwa sasa maafisa wakuu wa jimbo hilo wamesafiri kwenda eneo la ajali kufahamu zaidi kuhusu idadi rasmi ya waliofariki na watu ambao walikuwa ndani ya boti hilo.
Bw Iluka ameambia mwandishi wa BBC Mbelechi Msochi kwamba Idadi rasmi ya waliofariki bado haijajulikana na uchunguzi unaendelea.


                    YALIYOJILI